Monday, October 1, 2012

KONGAMANO KUBWA LA VIJANA LILOPEWA JINA LA CALL TO HIGHER DIMENSION KUFANYIKA JMOSI HII




  1. Kanisa la Word Alive Sinza linaloongozwa na Askofu Deogratius Lubala lililoko Sinza Mori jijini Dar es salaam, limeandaa kongamano la kipekee la siku mbili litakalowahusisha vijana kutoka sehemu mbalimbali. Kwa mujibu wa waandaaji wa Kongamano hilo, kongamano hilo litafanyika jumamosi ijayo na jumapili (Tarehe6-7/10/2012) kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa kumi na moja jioni ambapo chakula kitatolewa bure.Siku ya Jumapili kuanzia saa tisa mchana Kongamano litamalizika kwa IBADA KUBWA ya kusifu na kuabudu.

    Kongamano hilo la vijana litakuwa likifanyika kila mwaka na kwa mwaka huu limebeba ujumbe usemao “CALL TO HIGHER DIMENSION”.Vikundi mbalimbali vya uimbaji vitahudumu vikiongozwa na Word Alive Praise Team.Kwa kijana yeyote ambaye ni mkazi wa jiji la Dar es Salaam hii si ya kukosa ukizingatia waalimu watakaohudumu Mungu ameweka hazina kubwa ndani yao kwa utukufu wa wake.Lets meet Sinza Mori jumamosi na jumapili.

    1.Rose Mushi
    2.Pastor Isaack Mallonga
    3.Pastor Daniel Musokwa
    4.Lilian Modesta Mahiga
    5.Pastor Deogratius Lubal 6.Ramsey Ngwelleja

Wednesday, September 26, 2012

SEMINA YA NENO LA MUNGU INAYOENDELEA VIWANJA VYA JANGWANI NA MTUMISH WA MUNGU MWL CHRISTOPHER MWAKASEGE

 Ikiwa ni siku ya nne ya semina ya neno la Mungu inayoendelea katika viwanja vya jangwani Dar es salaam
mtumishi wa Mungu Mwakasege anaendelea kukukaribisha kuja kijifunza neno la Mungu na kupokea muujiza wako , anaendelea kuwa karibisha wakazi wote wa Dar lakini pia unaweza kuungana nae popote pale ulipo duniani kupitia radio na website hizo hapo chini ,
 !!Karibu ujiunge nasi kusikiliza neno la Mungu inayoendelea hapa jijini Dar es salaam kupitia redio wapo,redio sauti ya injili,redio upendo,www.mwakasege.org,www.kicheko.com na www.sautiyainjili.org.Semina itarushwa live kwanzia saa kumi hadi saa kumi na mbili jioni,kwanzia tarehe 23 September 2012 hadi jumapili tarehe 30 september 2012.Mwambie na mwenzako!Mungu awabariki!!

Saturday, August 25, 2012

SENSA KWA MAENDELEO JIANDAE KUHESABIWA KUANZIA USIKU WA LEO

Senhi sa ya watu na makazi kwa ajiri ya maendeleo ya nchi na wananchi itaanza
rasmi leo katika maeneo yote ya Tanzania wito wa serikali kwa jamii ni kuwasihi
kutoa ushirikiano ili kuhakikisha wanapata idadi kamili ya wananchi wake lakini
pia na wageni wanaoishi ndani ya Tz.
jamii inaombwa kutoa ushirikiano wa kutosha kwa kukuballi kuhesabiwa mara moja
na pia kutoa idadi ya kweli ili kuhakikisha zoezi hili litakalo dumu ndani ya siku  saba
kufanikiwa na bila kuwa na vipingamizi vyovyote.
pia serikali inatoa wito kwa viongozi wa dini kuwahamasisha waumini wao kushiriki
katika zoezi zima lakuhesabiwa na bila kuhusisha imani za kidini katika zoezi hili.

Wednesday, August 22, 2012

SENSA YA WATU TANZANIA USIKU WA TAR 25 KUAMKIA 26

Je Utamjuaje Karani wa sensa? Karani wa sensa atafika katika eneo la kuhesabiwa watu akiwa na kitambilisho na atakuwa amevaa sare maalum zitakazomtambulisha. Vile vile atakuwa ameongozana na kiongozi wa eneo unaloishi.

Saturday, August 11, 2012

KWA WAKAZI WA ARUSHA NA VITONGOJI VYAKE

Conference na mkutano mkubwa wa injiri mjini arusha unatarajiwa kufanyika kuanzia
tar 14-19 agosti mwaka huu '

KILICHO JILI LEO KWENYE LOVE TANZANIA FESTIVAL

                                                      Mtumishio wa Mungu Andrew Palau
                            Masanja mkandamizaji akishambulia jukwa la Tanzania Love Festival
          Mwimbaji Don Moen akisifu na kuabudu na umati wa watu waliofika   kwenye viwanja vya Jangwani