Kanisa
la Word Alive Sinza linaloongozwa na Askofu Deogratius Lubala lililoko
Sinza Mori jijini Dar es salaam, limeandaa kongamano la kipekee la siku
mbili litakalowahusisha vijana kutoka sehemu mbalimbali. Kwa mujibu wa
waandaaji wa Kongamano hilo, kongamano hilo litafanyika jumamosi ijayo
na jumapili (Tarehe6-7/10/2012) kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa kumi
na moja jioni ambapo chakula kitatolewa bure.Siku ya Jumapili kuanzia
saa tisa mchana Kongamano litamalizika kwa IBADA KUBWA ya kusifu na
kuabudu.
Kongamano hilo la
vijana litakuwa likifanyika kila mwaka na kwa mwaka huu limebeba ujumbe
usemao “CALL TO HIGHER DIMENSION”.Vikundi mbalimbali vya uimbaji
vitahudumu vikiongozwa na Word Alive Praise Team.Kwa kijana yeyote
ambaye ni mkazi wa jiji la Dar es Salaam hii si ya kukosa ukizingatia
waalimu watakaohudumu Mungu ameweka hazina kubwa ndani yao kwa utukufu
wa wake.Lets meet Sinza Mori jumamosi na jumapili.
1.Rose Mushi
2.Pastor Isaack Mallonga
3.Pastor Daniel Musokwa
4.Lilian Modesta Mahiga
5.Pastor Deogratius Lubal 6.Ramsey Ngwelleja
No comments:
Post a Comment