Thursday, June 21, 2012



                                                                                                                                                                MWNJILISTI Kabula George, anatarajia kugawa DVD za albamu ya Nitang’ara Tu kwa kila mtu atakayeingia kwenye Ukumbi wa kanisa la TAG Magomeni Mikumi Julai 8, mwaka huu wakati wa uzinduzi wake.

Akizungumza na gazeti hili Dar es Salaam jana, Mwinjilisti Kabula alisema ameamu kuweka utaratibu huo, ili kila mtu atakayeingia ukumbini humo aondoke na DVD kwa kuchangia kiasi cha sh. 5,000.

Mwinjilisti Kabula alisema tayari DVD hizo tayari zinapatikana katika maduka mbalimbali yaliyoteuliwa jijini Dar es Salaam.

DVD hizo pia zinapatikana katika mikoa mbalimbali ukiwemo Mwanza, Arusha, Dodoma na Kahama mjini.

Amewataka mashabiki wake kununua DVD halisi ili wanufaike na ubora wa nyimbo hizo, ambazo zinamafundisho kwa kila anayeziangalia

No comments:

Post a Comment