Thursday, June 21, 2012






Hatimaye kamati inayoandaa tuzo za Muziki wa Injili barani afrika siku ya jana imetoa orodha ya wanamuziki ambao watakuwa wakichuana katika kutafuta washindi wa Kategori mbalimbali.Kwa mujibu wa kamati hiyo mwanamuziki nguli kutoka Tanzania Mwanamama Christina Shusho amefanikiwa kuwa mwanamuziki PEKEE kutoka Tanzania aliyechaguliwa kuingia katika tuzo hizo mwaka huu na ameibuka katika kategori mbili ambazo ni Mwamamuziki bora wa Afrika Mashariki pamoja na mwanamuzik bora wa Kike Barani Afrika.

Christina Shusho, mwaka jana aliingia katika kategori ya mwanamuziki bora wa Afrika mashariki lakini hakufanikiwa kuingia kuibuka mshindi huku mwanadada Emmy Kosgei kutoka Kenya akichukua ushindi katika kategori hiyo.Tofauti na nchi nyingine za Afrika mashariki, kenya imetoa washindani wengi katika kategori mbalimbali.Kategori zinazoonekana kuwa na mpambano mkali ni pamoja na Mwanamuziki bora wa kike na wa kiume barani afrika,Album bora barani Afrika,na mwanamuziki bora kutoa nchi za kusini mwa Afrika ambapo kuna members wa Joyous celebration wakichuana na nguli wengine wa nchi hiyo.Tuzo hizi zinararajiwa kufanyika tar 7 July jijini London nchini Uingereza.


FEMALE ARTIST OF THE YEAR
Kefee -Nigeria
Onos Ariyo- Nigeria
Emmy Kosgei-Kenya
Dena Mwana – Congo
Ntokozo Mbambo- South Africa
Rebecca- UK
Gifty Osei- Ghana
Diana Hamilton-UK
Christina Shusho -Tanzania
Lara George- Nigeria


ARTIST OF THE YEAR- EAST AFRICA
Eko Dydda- Kenya
Emmy Kosgei - Kenya
Exodus- Uganda
Christina Shusho- Tanzania
Lam Lungwar- South Sudan
Sarah K- Kenya
Dawit Getachew-Ethiopia
Kambua-Kenya
Willie Paul- Kenya
Ann Marie Mutesi - Burundi

ALBUM OF THE YEAR
Blessing-Diana Hamilton (UK)
Ololo - Emmy Kosgei (Kenya)
Skuulfoo- Chapter 1 (Ghana)
Colours of Africa- Sonnie Badu (UK)
Crown Him King-Israel Mosehla (South Africa)
Mwamba Mwamba- Solly Mahlangu (South Africa)
Declaring his Name- Muyiwa and Riversongz (UK)
Overflo- Florocka (Akinwunmi Nathan Akiremi) (Nigeria)
Prophecy-Ohemaa Mercy (Ghana)
I Believe – Rebecca (UK)

No comments:

Post a Comment