Saturday, September 10, 2011


meli ya LTC Spice Islander iliyotokea huko Zanzibar usiku wa jana imezama

Meli hiyo inasemekana ilikuwa na abiria wapatao 610 ambapo juhudi za kuokoa majeruhi wa ajali hiyo zinaendelea hivi sasa.

Akizungumzia ajali hiyo, Naibu Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu, Issa Haji Ussi amesema tukio hilo limetokea saa 8:30 za usiku.

Haji Ussi amesema meli hiyo iliondoka katika Bandari ya Malindi Unguja ikiwa katika hali ya uzima, lakini katikati ya safari ikapata hitilafu na kusababisha kubinuka na hatimaye kuzama kabisa.

Hadi sasa haijaweza kufahamika idadi kamili ya watu waliofariki, lakini vyombo vya uokozi vimefika katika eneo la tukio kutoa msaada.

Naibu Waziri Issa amesema Serikali kwa kushirikiana na vyombo vya usafiri vya binafsi kama boti ziendazo kasi vimekwenda eneo la tukio kutoa msaada. Jeshi la Polisi Tanzania limetuma Helikopta yake kwenye eneo la tukio.

Awali, amesema Mamlaka zinazohusika zilipata taarifa za kuzama kwa meli hiyo baada ya Meli ya Mv Jitihada inayomilikiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuripoti kuzama kwa meli ya Spice Islanders ambayo ililazimika kukatisha safari yake kuelekea Kisiwani Pemba na kwenda kwenye tukio. Serikali imesema taarifa zaidi zitakuwa zikitolewa na wananchi wameombwa kuwa watulivu.







Meli hiyo inasemekana ilikuwa na abiria wapatao 610 ambapo juhudi za kuokoa majeruhi wa ajali hiyo zinaendelea hivi sasa.
Akizungumzia ajali hiyo, Naibu Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu, Issa Haji Ussi amesema tukio hilo limetokea saa 8:30 za usiku.
Haji Ussi amesema meli hiyo iliondoka katika Bandari ya Malindi Unguja ikiwa katika hali ya uzima, lakini katikati ya safari ikapata hitilafu na kusababisha kubinuka na hatimaye kuzama kabisa.
Naibu Waziri Issa amesema Serikali kwa kushirikiana na vyombo vya usafiri vya binafsi kama boti ziendazo kasi vimekwenda eneo la tukio kutoa msaada. Jeshi la Polisi Tanzania limetuma Helikopta yake kwenye eneo la tukio.
Awali, amesema Mamlaka zinazohusika zilipata taarifa za kuzama kwa meli hiyo baada ya Meli ya Mv Jitihada inayomilikiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuripoti kuzama kwa meli ya Spice Islanders ambayo ililazimika kukatisha safari yake kuelekea Kisiwani Pemba na kwenda kwenye tukio. Serikali imesema taarifa zaidi zitakuwa zikitolewa na wananchi wameombwa kuwa watulivu.












Thursday, August 18, 2011

Wednesday, August 17, 2011

Tuesday, August 16, 2011

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgeu5Tt7_7ePtgHg9HuLqBqcTeCNtEQ-3FuEj-Mp8T3Ge4looOUXJPioFIb8vHyS0jrud6FqSl2kxOlUN8XVqCs18VBNl_W70Sk1y7qK9JCnJc8m8mpO-GltyDJCKRsz_fnbKazvKSuRrQV/s400/PM.jpg

PETER MSECHU (TANZANIA) - WINNER TUSKER ALL STARS - 2011

Shindano la Tusker All Stars lililoanza 26 June,2011 limefikia fainali jana tarehe 14 August,2011 kwa washindi watatu kupatikana

Alpha Rwirangira toka Rwanda (TPF 3 - Winner),Peter Msechu toka Tanzania (Mshindi wa 2 – TPF 4) na Davis Ntare toka Uganda (TPF 4 – Winner) wameibuka washindi na wamepata shavu la kupiga show same stage na wasanii wa kimataifa baadaye mwaka huu nchini Kenya....

Washiriki wengine walikua Hemedi Suleiman toka Tanzania,Caroline Nabulime na Amileena Mwenesi toka Kenya,Bernard Ng'ang'a na Patricia Kihoro toka Kenya walishiriki na walikaa wiki 8 na Ma Mc walikua ni Prezentaz maarufu Eve D'Souza toka Kenya na Gaetano Kagwa toka Uganda na mbali na washindi hao 3 kupata shavu la ku-share stage moja na wasanii wa kimataifa,haijafunguliwa kama watapata zawadi au vp....!